
Zuwena Mohamed ‘Shilole’(kulia) na Mchungaji.

“Aisee ilikuwa noma, nilipoona ananiita nilishtuka kidogo. Mbaya zaidi aliniambia anataka tupige picha pamoja, ndipo alipoanza kunipa darasa la wokovu.
“Alinitaka nibadilike kimavazi, pia nisimsahau Mungu katika maisha yangu yote na alimalizia kwa kunitaka niende kanisani kwake ili ikwezekana nitumie uimbaji wangu kuwabadilisha wengi waweze kumtumaini Bwana,” alisema Shilole staa wa wimbo Nakomaa na Jiji.
Hata hivyo, katika mazungumzo hayo, Shilole alionekana kuguswa na maneno ya mchungaji huyo na kusema yamemkumbusha suala la kumkumbuka Mungu kila wakati katika kazi za mikono yake.
Akasema kwa kuzingatia hilo, sehemu ya mapato yake atakuwa akiyatumia katika kutoa sadaka husan kwa watu wasiojiweza ili kutimiza amri ya Mungu. “Ni wakati wa kubadilika, huu muziki tunafanya upo na utaendelea kuwepo lakini jambo la muhimu sana ni kumuabudu Mungu katika siku zote za maisha yetu ya hapa duniani,” alisema Shilole.