
Amacho kimenishangaza ni uamuzi wa Mjomba Mpoto... Nadhani ingefaa sana kama angekuwa neutral ili kulinda heshima ili raia kuona connection sanaa anayoifanya na dhamira halisi ya moyo wake.. Wako watu wengi wametunza siri za uanachama wao kwa vyama vyao ili kuendelea kunufaika na makundi yote katika jamii.
Politics is a game of opportunity, labda ameona fursa mahali.. Najua Sugu ameinspire wengi na ofcourse Chadema wamenufaika sana nae japo ni mmoja tu, Afande Sele anafanya vizuri pia akiishi aliyokuwa anahubiri.. Prof J pia nk.

Tukio limenikumbusha namna Nakaaya na Marlaw walivyokosea hesabu....
Nadhani misingi, nidhamu na heshima ya siasa zetu imeshusha hadhi na dhamana ya uongozi wa kisiasa. Kila mtu sasa akiwa maarufu tu utasikia anataka kuwa mbunge mahali fulani, hii ni bila kujali chama gani...
Ubunge umekuwa dili kutafuta utajiri wa haraka badala ya dhamana ya kuwakiliaha raia. Urais ndio umefanywa rahisi kila mtu anahisi anaweza kuwa rais.
Credit:Bongoclan