Habari Mpya

SOMA STORY HII YA KUSISIMUA | KAHABA KUTOKA BARA ASIA ~ CHINA...BONGE LA STORY..SOMA BILA KUKOSA..!!


Njia nzima Rose alikuwa na mawazo, hakuamini kama ule ndio ulikuwa mwisho wa kukaa nyumbani kwao. Hakutaka kurudi tena, hakutaka kuwasiliana na ndugu yeyote yule kutoka nyumbani kwao, kitu ambacho alikuwa akikitaka kwa wakati huo ni kuondoka na kwenda kuishi mbali. Bado alikuwa akifikiria mengi, hasa kutokana na ujauzito ambao alikuwa nao katika kipindi hicho, haukuonekana kuwa sababu ya yeye kuendelea kuishi ndani ya nyumba ile.
Leo baba yake alikuwa ameamua kwenda kumuua Irene, ile ilimaanisha kwamba ingewezekana siku nyingine kuamua kumuua hata yeye mwenyewe. Alitaka kuwa makini kwa kila hatua ambayo ilikuwa inatokea, alitakiwa kuwa makini kwa kila kitu ambacho alitakiwa kukifanya.
Ndani ya jiji la Dar es Salaam alikuwa na ndugu wengi lakini katika kipindi hicho aliona asingeweza kwenda kwa ndugu yeyote yule zaidi ya Irene ambaye nae alionekana kuwa adui wa familia yake. Safari bado ilikuwa ikiendelea kuelekea Sinza Makaburini, katika kipindi hicho alikuwa akitaka kuonana na msichana Irene na kumwambia kwamba alikuwa ameamua kuondoka nyumbani kwao.
Safari wala haikuwa ndefu sana, wakafika Sinza Makaburini ambapo akamlipa dereva bajaji kiasi cha fedha alichokuwa akikihitaji na kisha kuanza kuifuata jengo la hosteli ile, alipolifikia akafungua geti na kuingia ndani. Wasichana wengi walikuwepo ndani ya eneo lile wakifua wengine wakiwa na mataulo wakielekea bafuni kuoga.
“Samahani. Irene nimemkuta?” Rose alimuuliza dada mmoja ambaye alikuwa akifua.
“Irene yupi?” Msichana yule aliuliza.
”Irene Godfrey”
“Mmmh! Sijui. Nenda katika chumba chake ukamuulizie” msichana yule alimwambia Rose
“Chumba chake kipo wapi?” Rose aliuliza.
Hapo ndipo ambapo yule msichana alipoanza kumuelekeza Rose chumba cha Irene kilipokuwa na kisha Rose kuanza kupiga hatua kuelekea alipoelekezwa. Alipoufikia mlango, akaanza kupiga hodi na kisha kufunguliwa. Wasichana kadhaa walikuwa ndani ya chumba hicho wakijiandaa kuelekea vyuoni.
“Samahani” Rose alisema mara baada ya salamu.
“Karibu” Msichana mmoja alimwambia Rose.
“Irene nimemkuta?”
“Hayupo”
“Kaelekea wapi?”
“Aliondoka toka jana. Hakutuaga. Ila si umpigie simu” Msichana yule alimwambia Rose.
Hapo hapo Rose akachukua simu yake na kisha kuanza kumpigia Irene, simu haikuita sana, ikapokelewa na sauti ya kichovu ya Irene kuanza kusikika. Waliongea kwa dakika kadhaa, Rose akatakiwa kuelekea Mwananyamala A alipokuwa Irene. Rose hakutaka kuendelea kubaki mahali hapo, alichokifanya ni kuaga na kisha kuondoka mahali hapo. Alipofika nje, akakodi bajaji na kuondoka.
Safari ya kuelekea Mwananyamala A ikaanza , mpaka pale ambapo alipofika Mwananjamala A na kumuona Irene ambaye alikuwa akimsubiri. Wakakumbatiana kwa furaha na kisha kuanza kuondoka mahali hapo. Safari hiyo ikaishia katika chumba cha Asha, chumba ambacho kilionekana kukaliwa na mtu msela kutokana na mpangilio wake kutokuwa wa kuvutia.
“Imekuwaje tena?” Irene alimuuliza Rose.
“Nilikimbia nyumbani. Nilihofia kwamba kama baba amegundua nimekupigia simu, hasira zake zingeishia kwangu” Rose alimwambia Irene.
“Pole sana. Kwa hiyo hautorudi tena?”
“Siwezi kurudi”
“Dah! Haina jinsi. Ngoja nikufanyie mishemishe ya mjini hapa ukakae katika chumba kimoja nilipanga hapo Kinondoni ila sijakitumia sana na kuhamia hosteli. Kama miezi sita imebaki mpaka kodi kumalizika. Unaonaje? Au utashindwa kukaa peke yako?” Irene alimwambia Rose.
“Hakuna tatizo” Rose alijibu.
Irene hakutaka kuchelewa sana, akaoga na kisha wote kwa pamoja kuanza safari ya kuelekea Kinondoni na kisha kuelekea katika chumba hicho. Walipofika, wakaingia ndani na kisha kuanza kukifanyia usafi kutokana na fumbi kuwa jingi ndani ya chumba hicho.
Chumba kilionekana kuwa kikubwa, kilikuwa na kila kitu, makochi makubwa, kitanda pamoja na jiko la gesi bila kusahau televisheni ambayo ilikuwa katika stendi yake. Kwa kiasi fulani, chumba kile kilionekana kumvutia Rose ambaye akaridhika kwa moyo mmoja kukaa ndani ya chumba kile.
Hapo ndipo ambapo Rose akaanza maisha, mara kwa mara Irene alikuwa akifika hali hapo kwa ajili ya kumuona na pia kumfanyia usagaji. Katika kipindi hiki Rose akaonekana kubadilika sana, hakutaka kufanyiwa mchezo wa usagaji, alikuwa amekwishaamua kwamba alikuwa ameuacha mchezo huo kwa sababu tu alikuwa mjauzito katika kipindi hicho.
Irene alibaki kumshangaa, hakuamini kama kulikuwa na msichana ambaye alikuwa akiufanya mchezo ule na kisha kubadilika na kuamua kuuacha kabisa. Hilo likaonekana kuwa tatizo kwa Irene, mara kwa mara alikuwa amimshawishi Rose lakini wala hakuonekana kukubaliana nae, alikuwa ameamua kubadilika kwa asilimia mia moja.
Irene hakuonekana kufahamu kile ambacho kilikuwa kikiendelea kwa Rose, hakufahamu kama binti huyo katika kipindi hicho alikuwa mjauzito. Kwake, alimuona kuwa msichana wa kawaida sana ambaye wala hakuwa na kiumbe chochote tumboni mwake.
“Kwa nini lakini mpenzi?” Irene alimuuliza Rose kwa sauti ya unyonge.
“Hapana. Nimeaua tu” Rose alijibu.
“Hakuna mtu anayeamua kitu bila sababu. Kutakuwa na sababu tu”
“Nina mimba. Hiyo ndio sababu yenyewe” Rose alitoa jibu liliomfanya Irene kushtuka.
“Una mimba? Ya nani? Imekuwaje tena?” Irene aliuliza huku akionekana kushtuka.
“Nimepata mimba Irene”
“Kivipi.Uume wa bandia umekupa mimba?”
“Hapana. Nimepewa mimba na Joshua” Rose alijibu.
Hapo ndipo ambapo Rose akaamua kumhadithia Irene kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea katika maisha yake katika kipindi ambacho alikuwa nyumbani. Ile ikaonekana kuwa stori mbaya kwa Irene ambaye alikuwa makini akimsikiliza tu. Hakukuwa na kitu kilichobadilisha ukweli katika kipindi hicho, Rose alikuwa mjauzito na kwa mbali tumbo lilikwishaanza kuonekana.
“Kwa hiyo ndio basi tena?” Irene aliuliza kwa sauti ya upole.
“Haina jinsi. Itabidi iwe hivyo” Rose alijibu.
“Sasa itakuwaje kwa Peter ambaye anaamini mimba ni yake?”
“Bado sijajua. Sitaki kufikiria hilo kwa sasa. Acha nifanye mambo yangu kwanza” Rose alimwambia Irene.
****
Terry alikuwa kimya huku akiifanya kazi yake ambayo aliambiwa aifanye katika kipindi hicho. Aliambiwa azitoe fedha zote na kubakisha kiasi cha dola milioni mbili ambazo hizo zingebaki na kisha Bwana Zhan kufanyia mambo yake. Kama alivyosema, zoezi wala halikuwa kubwa, ni ndani ya dakika nne tu tayari zoezi zima lilkuwa limekamilika.
Hiyo ikaonekana kuwa furaha kwa Bwana Zhan ambaye akaamua kula chakula cha mchana na Terry na kisha kumfanyia mipango ya usafiri wa ndege kwa ajili ya kurudi nchini Marekani huku akitaka kila kitu kiwe siri yao na asiambiwe mtu yeyote, kwa maana hiyo siri ingekuwa kwa Bwana Zhan, Terry pamoja na mke wa Bwana Zhan, Lucy.
Bado kulikuwa na mambo mengi ya kufanya kwa wakati huo, bado aliona kwamba kulikuwa na kitu kimoja ambacho alitakiwa kukifanya kwa wakati huo, kutoroka na kuelekea nchini Tanzania bila kugundulika. Hiyo haikuonekana kuwa rahisi kufanyika, alitakiwa afanye kitu kitu kimoja ambacho kingemfanya kutokujulikana na mtu yeyote kama alikuwa yeye.
Wazo moja likamjia kichwani, wazo lile likaonekana kustahili sana kuchukuliwa hatua, kwa moyo mmoja, akaamua kutengeneza sura za bandia ambayo angeitumia kusafiria mpaka nchini Tanzania pamoja na mke wake. Kwa haraka bila kupoteza muda akaanza kuwasiliana na wachongaji wa sura za bandia na ndani ya masaa mawili walikuwa ndani ya nyumba hiyo na kisha kuanza kuwapa maelekezo juu ya nini kilitakiwa kufanyika mahali hapo.
Kiasi kikubwa cha fedha kilihitajika kwa ajili ya kukamilisha kila kitu ambacho alikuwa akitaka kifanyike na ndani ya siku mbili, tayari sura mbili za bandia zilikuwa zimekwishakamilika. Mpaka hapo kila kitu kilikuwa tayari na walipanga kwamba siku itakayofuatia ndio ilikuwa siku ya kuondoka nchini hapo na kuelekea nchini Tanzania. Usiku wakalala kitandani kwao huku sura za bandia zikiwa pembeni ili ikifika asubuhi wazivae na kisha kuanza kuitoroka nchi ya China.


Credit:-http://www.tanzanianewz.com/
SHUKA CHINI KUTOA MAONI YAKO
Designed By